Sunday 22 March 2015

TEZI DUME


TEZI DUME (PROSTATE GLAND)
Ni tezi ambalo linapatikana kwa wanaume tu kwenye mifumo ya uzazi chini ya kibofu cha mkojo.Kuna njia ambayo inaitwa urethra ambayo imeunganika kwenye uume ambayo inapitisha mkojo kutoka nje.huwa inapitia kwenye tezi dume.Tezi dume ni muhimu sana kwenye uzazi wa mwanaume kwa sababu huwa inazalisha fluid au majimaji ambayo yanasaidia kulinda na kulisha mbegu za kiume .Mbegu hizi huwa zinapitia mirija maalum ambayo inaitwa seminal vesicles kupitia ejaculatory tract hadi kufikia urethra.
Tezi dume huwa linachochewa kukaa katika hatua mbili tofauti:
(i)Tezi dume huwa linachochewa na hormone (sex hormone)kutoka  kwenye gololi za wanaume na kujenga hisia……(ndio maana castration(kuasiwa)unakosa hamu ya tendo la ndoa.
(ii)Hatua ya pili tezi dume huwa llinakua mwanaume anapofika umri wa miaka 30………
Wanaume wengi huwa wanaanza mabadiliko au matatizo ya kwenda haja ndogo umri unapoongezeka,ambayo huwa insababishwa na kutanuka kwa tezi dume,kumbuka kutanuka kwa tezi sio tatizo ambalo linasababisha mtu kukosa kwenda haja ndogo vizuri matatizo makubwa huwa ni cancer kwenye tezi.


DALILI
·        Kwenda haja ndogo mara kwa mara nyakati za usiku.
·        Kukojoa mara kwa mara wakati wa mchana.
·        Kutokwa na mkojo bila kujizuiya.
·        Unaenda kujisaidia haja ndogo lakini  unachukua muda mrefu mkojo kutoka.
·        Mkojo unatoka tone kadhaa mara tu unapomaliza kwenda haja.
·        Unakojoa karibu kiasi cha kuloanisha suruali.
·        Kusika kibofu kizito au kinachoma wakati wa kukojoa
·        Kukojoa kila baada ya muda mfupi.
MUONE DAKTARI
·        Unapohisi huwezi kukojoa.
·        Unaposikia maumivu makali
·        Unapoona damu kwenye mkojo.
·        Unapotokwa na usaha au mbegu za kimu wakati wa kwenda haja ndogo
·        Kushindwa kuzuia mkojo.
UVIMBE WA TEZI DUME’
Bacteria wakati mwingine huwa wanasababisha tezi dume kuvimba mtafute daktari.
·        Unaposikia maumivu ya mgongo
·        Maumivu chini ya kitovu
·        Kushindwa kuzuiya mkojo.
Kinachosababisha tezi dume kutanuka pia ni presha kupanda ,tezi dume linapotanukka au kukua zaidi ya saizi ya kawaida,mwanaume huwa anapata shida kukojoa wakati mwingine huwa wanatumia catheter.
Chanzo kingine cha kuongezeka kwa tezi dume ni misuli ya urinary bladder kutanua au kubadilika kuwa dhaifu.
EPUKA NA :-
·        Kunywa pombe,kahawa,vitu vya sukari n.k

UGONJWA WA HEMORRHOIDS/BAWASILI

                                          




UGONJWA WA HEMORRHOIDS/BAWASILI
Bawasili ni ugonjwa ambao unatokana na nyama kuota sehemu za haja kubwa ndani au nje ya haja kubwa.Ni mishipa ya damu (veins)ambayo huwa inavimba.Unaweza ukasikia maumivu,muwasho au kutokwa  na damu nyeusi au mbichi au au usaha wakati mwingine kutoka sehemu hizo za haja kubwa.tiba inategemea na dawa unazoweza kutumia,staili ya maisha yako au upasuaji.unapoona tatizo linaongezeka muone daktari haraka.
CHANZO NI NINI?
Bawasili inasababishwa presha kubwa sehemu za haja kubwa (rectum)hii preha huwa inatokana na:
·        Kufanya mazoezi magumu kwa kukandamiza sana tumbo.
·        Kukosa choo kwa muda mrefu(constipation)au kuharisha mara kwa mara kwa muda mrefu.
·        Upungufu wa uzito au uzito kuongezeka(obesity)
·        Wakati wa ujauzito(underweight).
·        Kuingiliwa kinyume na maumbile(homosexual).
·        Kukosa roughage
·        Kuumizwa uti wa mgongo.
·        Staili ya au kukaa ukiwa umeinama,.
Bawasili  huwa inatokea kwa watu ambao mishipa ya damu inatanuka sehemu za haja kubwa.

DALILI.
Dalili huwa zinategemea na sehemu iliko bawasili.Inaweza iwe ndani ya haja kubwa au nje ya  haja kubwa.
Bawasili ya ndani ya haja kubwa huwa inauma ndani kwa ndani na wakati mwingine haitambuliki mapema.Lakini wakati wa kujisaidia haja kubwa inaweza ikachana ule uvimbe na kutoa damu au muwasho sana.
Bawasili ya nje huwa inajitokeza sehemu za haja kubwa kwa nje.huwa zinauma,kuwa au kutoa damu.Bawasili za nje hutokana na damu kujaa kwa mishipa na kusababisha uvimbe mkubwa,saizi ya yai la kuku.

BAWASILI YA NJE UTAITAMBUA KWA:
·        Kupata maumivu makali sehemu za haja kubwa wakati wa kukaa au kufanya mazoezi
·        Kupata muwasho sehemu za haja kubwa.
·        Damu mbichi zu nyeusi kwenye kinyesi
·        Uvimbe sehemu za haja kubwa.
Dalili za kutokwa na damu sehemu za haja kubwa ndo dalili mbaya sana kwa sababu inaweza ikazalisha tatizo linguine kama saratani mtafute daktari.
·        Unapotokwa na damu nyingi sehemu za haja kubwa.
·        Vidonda vinapotokea sehemu za haja kubwa
·        Unatambua kinyesi kuwa na damu nyeusi
TIBA
·        Muone daktari
·        Tumia cream lotion au osha sehemu hiyo na maji ya moto mara tatu kwa siku.
·        Tumia dawa za maumivu kama paracetamol.
KUZUIA
·        Hakikisha unapata choo kilaini.kukosa choo au kupata choo kigumu kunachangia sana tatizo hili.
Mambo yafuatayo yanaweza yakakusaidia kuepukana na bawasili.
·        Kula vyakula ambavyo vina fibre(roughage)mboga za majani
·        Kunywa maji ya kutosha
·        Unapoenda haja kubwa usijikamue sana
·        Usikae  muda mrefu ukiwa umezuia haja kubwa.
·        Pata mazoezi ya kutosha
·        Epukana na kukaa muda mrefu kila siku bila kunyanyuka.
 

MAGONJWA YA ZINAA

                                                         MAGONJWA YA ZINAA                

                                                               MAGONJWA YA ZINAA


MAGONJWA YA ZINAA
Magonjwa ya zinaa ni magonjwa ambayo yanasambazwa kupitia kujamiiana.Mtu mmoja aliyeambukizwa anaweza kusambaza kwa mtu mwingine ambaye hajaambukizwa.Yanawezwa kuambukizwa kupitia ukeni au sehemu za haja kubwa kwa wale ambao wanajamiana kupitia sehemuza haja kubwa.
VISABABISHI VYA MAGONJWA YA ZINAA NI:-
·        Virus kama HIV au hepatitis B
·        Bacteria kama kisonono na kaswende,
Ni nani ambaye anaweza kupata magonjwa haya?
Mtu yeyote ambaye anajihusisha na kujamiiana na mtu mwingine ambaye ana magonjwa haya.mf wa
·        Watu ambao wana wapenzi wengi
·        Mtu ambaye anamapenzi ambaye amewahi kuwa na wapenzi wengi.
·        Watu ambao hawatumii condom wakati wa kujamiiana.
·        Watu ambao wana wapenzi na hao wapenzi wana mahusiano sehemu nyingine na hawatumii condom wakati wa kujamiiana.
·        Watu ambao wanajiuza(wanaume na wanawake).
·        Watumiaji wa madawa ya kulevya na hachukui tahadhari kwenye swala la kujamiiana.
DALILI ZA STD
·        Dalili huwa zanategemeana na aina ya maambukizi.mfano
·        Usaha kutoka kwenye uume wa mwanaume au uke wa mwanamke.
·        Muwasho mkali sehemu za siri.
·        Maumivu makali wakati wa kujamiiana au waakati wa kwenda haja ndogo.maumivu yanawea yawe ya kuchoma.
·        Upele mwekundu unaweza kujitokeza sehemu za siri,haja kubwa,mdomoni,ulimi na kooni.
·        Maumivu makali sehemu za haja kubwa wakati wa kujisaidia hususani wale ambao wanajamiiana sehemu za haja kubwa.
·        Malengelenge yanaweza yajitokeze sehemu za siri.
·        Wakati mwingine ngozi ya mkononi na miguuni inaweza kutokkewa na mabakamabaka.
·        Mgonjwa atapata homa kali,mwili kuchoka,nyama za mwili kuuma na matezi kujitokeza.
·        Maambukizi kupitia hepatitis yanaweza yasababishi mkojo kuwa mzito au wa njano na kinyesi kubadilika kwa rangi ya cheki nyeupe macho,kucha na ngozi hubadilika kuwa rangi ya njano.
Kwa wale ambao wameambukizwa virusi vya ukimwi wanaweza kupungua uzito wa mwili,maambukizi ya magonjwa ya mara kwa mara,jasho usiku,kuchoka sana na upele au malengelenge kwenye ngozi na ulimi.n.k