Sunday 22 March 2015

UGONJWA WA KICHOCHO

                              

UGONJWA WA KICHOCHO/BILHARZIA



                                                         


KICHOCHO/BILHARZIA
·        Ni ugonjwa ambao unatokana na minyoo midogo ya aina ya schistosoma kuingia mwilini na kusababisha muwasho katika viungo mbalimbali unaosababisha homa,udhaifu,kupungukiwa ma kinga mwilini hadi kutokea kansa na kifo.
·        Minyoo ya aina ya schistosoma inatokea katika konokono za maji kwa hali ya lava(larvae stage)larvae zinatoka kwenye konokono na kutembea katika maji karibu nayo zikitafuta wanyama au awtu wanapolenga kuingia ili waendelee kukua katika miili  yao.zinatoboa ngozi na kutembea na kuingia hadi  mishipa ya damu hadi maini zinapobadilika kuwa minyoo yenye urefu wa milimita1-2,minyoo inaendelea kutembea mwilini hadi kufikia utumbo,mapafu au ubongo.Huwa zinasababisha vurugu katika viungo hivi na kusababisha mzio unaonekana kwa njia ya homa .Minyoo inataga mayai yanayotoka mwilini kwa njia ya kibofu na mkojo.
·        Kama mkojo unaachishwa kwenye maji,mayai hubadilika kuwa larvae zinazoingia katika konokono na mzunguko unaanza upya.
·        Kwa hiyo njia  ya kuambukizwa ni kuingia katika maji penye konokono zilizoambukizwa..siku hizi karibu kila ziwa,bwawa au maji ya vidimbwi huwa na hatari ya kichocho.
DALILI
Kichocho ni ugonjwa ambao ni chronic.wagonjwa wa kichocho huwa wanakabiliwa ana anemia na utapia mlo.kichocho kinaweza kuonekana wiki chache baada ya maambukizi.
·        Utasikia tumbo linauma sana
·        Kikohozi kisichoisha
·        Kuharisha mara kwa mara (damu)
·        Homa kali
·        Kizunguzungu
·        Ini kuvimba pamoja na bandama
·        Ongezeko kubwa la seli nyeupe
·        Maambukizi kwenye ngozi ambayo yanasababisha muwasho miguuni na sehemu zingine za mwili.
·        Muwasho sehemu za siri na kutokea vidonda ambavyo vinaweza kuwa njia kuu ya maambukizi ya ukimwi.
·        Mayai yanaweza kusambaa hadi uti wa mgongo na kusababisha ugonjwa wa akili
·        Wakati mwingine ugonjwa huu unasababisha uvimbe kwenye kizazi,matokeo yake mgonjwa anapata
Presha ya kupanda au kushuka,matatizo ya figo.

0 comments:

Post a Comment